hk CONTACTS

hk CONTACTS

Monday, October 7, 2013

HIVI NDIVYO AJALI MBAYA ILIVYOPOTEZA UHAI WA MMILIKI WA CLUB ZA MATEMA NA JACARANDA, HAIKUWA RAHISI KUTOKA MTU AKIWA HAI AU KUOMBA MAJI YA KUNYWA!!!



 Marehemu Robert Mwandisi enzi za uhaki wake na picha hizi alipiga siku moja kabla ya kifo chake.

 Haya ni mabaki ya sehemu ya gari hii ya thamani kubwa aina ya Lange Lover sport kama inayoonekana ambayo marehemu alikuwa kitumia kwenye shughuri zake za kazi.

Na Mwandishi Wetu
Mmiliki wa baa na Club za Matema Annex Park zenye umaarufu mkubwa Jijini Dar hasa Kinondoni aliyehamika kwa jina la Robert Mwandisi amepoteza maisha baada ya kupata ajali mbaya maeneo ya Daraja Mbezi Chini kwenye daraja la Kawe.
Xdeejayz ambayo imefika kituo cha polisi Oysterbay na kushuhudia gari hiyo aina ya  Range Lover Sport yenye namba za usajili T660 CEP ikiwa imeharibika vibaya kwa hali ya muonekano wa gari hiyo isingekuwa rahisi kutoka mtu akiwa salama.
Habari zaidi kuhusu chanzo cha ajali hiyo iliyotokea saa kumi za usiku ambapo wakati marehemu akifikwa na balaa hilo alikuwa akitokea kwenye mizinguko ya biashara zake na alikuwa kirejea nyumbani kwake mbezi beach na alipofika maeneo hayo gari yake ambayo ilielezwa ilikuwa kwenye kasi kubwa iliacha njia na kupinduka zaidi ya mara sita hali iliyosababisha ijikunje kama chapatti.
Hata hivyo meneja Promotioni wa Club ya Jacaranda iliyopo maeneo ya Mango Garden aliyefahamika kwa jina la Maneno ametoa ratiba ya msiba wa marehemu bosi wake kama ifuatavyo

Siku ya Jumanne asubuhi Saa 2 kutakuwa na ibada ya misa ya kumuombea marehemu nyumbani kwake Mbezi,Baada ya misa litafuata tendo la kuuaga mwili wa marehumu baada ya shughur za kuaga kumalizika safari ya kuelekea Kyela Mkoani Mbeya itaanza na huko ndiko utakapoenda kupunzishwa mwili wake katika makao yake ya milele.
Marehemu Robart ameacha mjane mmoja na watoto wawili
Kwa niaba ya kampuni  Entertainment Masters Ltd na bodi ya wakurugenzi pamoja na wafanya kazi wote wa Club Maisha Mbeya, Dar, Ntwara, Mwanza na Dodoma wanaungana na familia ya marehemu kwenye kipindi hiki kigumu cha kuondokewa na ndugu yetu kipenzi kimsingi pengo lake halitozibika daima kwetu kwani tulishirikia na marehemu mambo mbalimbali ya kibiashara nk lakini kwa sasa hatuna budi kumshukuru mungu kwa kazi yake ambayo daima haina makosa.
MUNGU AMETOA NA SASA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE  MILELE AMEN

No comments:

Post a Comment