hk CONTACTS

hk CONTACTS

Tuesday, May 21, 2013

MCHEZA FILAMU ZA NGONO SEHEMU YA 9




Tayari mambo yalikwishaanza kuwa magumu kwa Gibso
n, simu ambayo alikuwa ameipokea kutoka kwa Daniel ikaanza kumtia kiwewe kupita kawaida. Hakutulia, muda wote alikuwa amkimsisitizia Katie kwamba ilikuwa ni lazima wauvunje mkataba wa ndoa yao ili aweze kuikoa nafsi yake ambayo ilikuwa ikisakwa sana.
Baada ya kulalamika sana, Katie akakubali kishingo upande. Moyoni mwake ilikuwa imemuuma kupita kawaida, mapenzi yake makubwa bado yalikuwa kwa Gibson ambaye kwa wakati huo alitaka wavuje mkataba wa ndoa wa miaka mitano ambao walikuwa wameandikishiana.
Walichokifanya ni kuelekea mahakamani ambako huko mkataba ukavunjwa. Ingawa Gibson alikuwa akifanya hivyo lakini moyo wake ulikuwa ukimuuma kupita kawaida. Nguvu ya fedha ndio ambayo ilikuwa imempelekea kufanya kitu kama kile ambacho wala hakuwa akitaka kukifanya.
“Nitarudi Tanzania tu. Tena haraka iwezekanavyo” Gibson alijisemea.
Alikaa nchini Marekani kwa siku mbili zaidi huku akionana na Daniel ambaye alikuwa akimpa pongezi kwa kile ambacho alikuwa amekifanya, na baada ya hapo, akakata tiketi na kurudi nchini Tanzania kwa kutumia ndege ya American Airlines.
Ndani ya ndege hakuwa na raha hata kidogo, kwanza akili yake ilikuwa ikimfikiria sana Katie ambaye alikuwa amemuacha katika hali ya unyonge mkubwa huku akiwa amemuumiza kupita kawaida. Ukiachilia na Katie, pia mawazo yake yalikuwa yakimfikiria mke wake aliyemuacha nchini Tanzania, Prisca pamoja na mtoto wake, Genuine.
Gibson hakujua kama Prisca alikuwa amekwishajua kilichoendelea au la. Kitu ambacho alikuwa akitaka kukifanya mahali hapo ni kuusoma mchezo tu. Kwanza angeangalia Prisca angempa mapokezi gani, hapo ndipo ambapo angegundua kwamba siri ilikuwa imevuja au bado iliendelea kuwa siri.
Alitumia zaidi ya masaa ishirini katika ndege ile na ndipo ndege ilipotua katika uwanja wa Mwl Julius Nyerere huku ikiwa ni saa tisa usiku. Kwa sababu ilikuwa ni usiku sana, Gibson hakutaka kurudi nyumbani, alichokifanya ni kwenda kulala kwenye hoteli ya New African.
Usiku wala hakulala, kichwa chake kilikuwa kikiwafikiria watu wawili kwa wakati huo. Kwa Katie, alijiona kufanya uamuzi mkubwa na mgumu kufanyika, kuna wakati mwingine alijiona bora amefanya uamuzi ule kwani ulikuwa na manufaa kuliko kuendelea kuishi na mwanake huyo ambaye alikuwa akicheza filamu za ngono.
Katika kichwa chake, kwa wakati mwingine alikuwa akimfikiria sana mke wake, Prisca. Hakujua mwanake huyo angesema kitu gani hasa mara baada ya kuishi nchini Marekani kwa zaidi ya miezi sita bila kuwasiliana nae. Akili yake ikaanza kufikiria uongo mbalimbali ambao alitakiwa kumwambia Prisca mara baada ya kufika nyumbani kwake.
“Nitamdanganya tu, wanawake ni rahisi sana kuukubali uongo” Gibson alijisemea.
“Mmmh! Lakini miezi sita bila mawasiliano! Hivi kama isingekuwa Daniel si mpaka mwaka ungetimia bila kufanya mawasiliano na Prisca. Kweli nilifanya kitu kibaya sana” Gibson alijisemea na kisha kupatwa na usingizi huku ikiwa imetimia saa kumi na mbili alfajiri.
Alikuja kuamka ikiwa saa saba mchana muda ambao aliagiza chakula na kuletewa chumbani na kisha kuanza kula. Kichwa chake kwa wakati huo kilikuwa kikifikiria namna ya kumwambia Prisca ili aweze kumuelewa. Ni kweli kwamba alitunga uongo mbalimbali lakini kwa wakati ho, kila uongo ambao alikuwa ameutunga ulionekana kutokufaa, yaani aliuona kuwa uongo wa kitoto.
Ilipofika saa tisa, akajitoa mhanga na kuanza kuelekea nyumbani kwake. Kadri gari ilivyokuwa ikizidi kusogea na ndivyo ambavyo wasiwasi ulivyokuwa ukimshika zaidi na kuufanya moyo wake kududa kupita kawaida.
Alichukua dakika thelathini hadi kufika nyumbani ambako akateremka ndani ya taksi na kisha kumlipa dereva na kuanza kulifuata geti la nyumba yake. Mapigo yake ya moyo yakazidi kudunda zaidi na zaidi kana kwamba kulikuwa na hatari kubwa mbele yake. Alipolifikia geti, akabonyeza kengele na mlinzi kuja kufungua.
“Karibu sana kaka” Mlinzi alimkaribisha huku akimpokea begi.
“Subiri kwanza. Shemeji yako yupo?” Gibson aliuliza hata kabla hajaingia ndani.
“Hayupo. Aliondoka kwenda kwa wazazi wake” Mlinzi alimjibu.
“Dah! Toka lini?”
“Mwezi wa tano huu” Mlinzi alimjibu Gibson jibu ambalo likaonekana kumtia wasiwasi.
“Duh! Kwa nini sasa?”
“Nilimsikia Rehema akisema kwamba kisa kilikuwa picha” 
“Picha gani?”
“Hakutaka kuniambia”
“Ok! Rehema mwenyewe yupo?”
“Ndio” Mlinzi alijibu.
Gibson akaanza kupiga hatua kuingia ndani na kisha kuufuata mlango wa kuingilia sebuleni. Kwa wakati huo alikuwa akitaka kuongea na Rehema ambaye alikuwa mfanyakazi wa ndani na kisha kumuuliza kuhusu picha ambazo mpaka hapo zikaonekana kumchanganya.
“Picha gani?” Gibson alimuuliza Rehema.
“Kuna picha alipewa zikionyesha kwamba ulipiga na mzungu” Rehema alijibu.
“Sasa kupiga picha na wazungu si kawaida sana hasa unapokuwa Marekani au Ulaya. Kipi hasa kilichomfanya kuondoka hapa nyumbani?” Gibson aliendelea kuuliza.
“Hizo hizo picha”
“Picha?”
“Ndio. Ulipiga ukiwa na mwanamke wa kizungu ambaye alikuwa amevaa shela la harusi huku wewe ukiwa umevaa suti, yaani lilionekana kuwa tukio la kufunga ndoa” Rehema alimwambia Gibson ambaye akabaki kimya.
Tayari kila kitu kiichoendelea nchini Marekani kikaonekana kujulikana kwa Prisca, kwa maana hiyo kama Prisca aliweza kuujua ukweli basi iliwezekana hata wakwe zake na wazazi wake walikuwa wakiufahamu ukweli. Kitu alichokifanya mahali hapo ni kutoka nje, kuchukua gari na kisha kuanza kuelekea nyumbani kwao huku akioneknana kuchanganyikiwa.
Tayari kwa wakati huo alijiona kufanya makosa makubwa, asingeweza kuelekea nyumbani kwa kina Prisca bila wazazi wake, alichokuwa akikifanya kwa wakati huo ni kumfuata baba yake, mzee Lyimo pamoja na mama yake ili waweze kuelekea nyumbani kwa kina Prisca kwa ajili ya kumuombea msamaha kwa kila kilichotokea nchini Marekani.
“Umefanya upumbavu mkubwa sana” Mzee Lyimo alimwambia Gibson kwa sauti ya juu.
“Nafahamu baba, nafahamu kwamba nimefanya kosa kubwa lakini ninahitaji kusamehewa pia kama ambavyo ninaomba msamaha” Gibson alimambia baba yake.
“Yaani umetutia doa hata sisi wenyewe. Tumeonekana tumekulea katika maisha ya ajabu ajabu. Eti unaondoka hapa na kuelekea Marekani kufunga ndoa, tena na mwanamke malaya ambaye anacheza filamu za ngono. Huo ni ujinga sana” Mzee Lyimo alisema maneno ambayo yalimfanya Gibson kushtuka.
Hapo ndipo alipogundua kwamba wazazi wake walikuwa wakifahamu kila kitu kilichoendelea na hadi kazi ambayo Katie alikuwa akiifanya ilikuwa imekwishagundulika. Kwake, tayari mambo yakaanza kuonekana kuwa magumu, alijua fika kwamba kwa hatua ile ambayo alikuwa amefikia, ilikuwa ngumu sana kwa Prisca kuweza kumsamehe.
Gibson akaanza kueleza kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika maisha yake pamoja na Katie, wazazi wake walikuwa kimya huku wakimsikiliza kwa makini kwani walihitaji kufahamu kila kitu kuona ni kwa namna gani wangeweza kuwaelezea wazazi wenzao ili kukubaliana nao na kumsamehe Gibson.
“Kwa hiyo ukaamua kuvunja mkataba wa ndoa?” Mzee Lyimo alimuuliza.
“Ndio. Niliamua kuuvunja kwa sababu nilijiona kuwa na uhitaji mkubwa wa kuja Tanzania na kumuona mke wangu na mtoto wangu. Kamwe nisingeweza kukaa zaidi bila kuwaona wao” Gibson alidanganya.
Gibson, mzee Lyimo na mama yake, Bi Yustina wakaanza kuelekea nyumbani kwa mzee Steven huku lengo lao likiwa ni kumuombea msamaha kijana wao ambaye alikuwa ameamua kutubu dhambi zake juu ya kile ambacho alikuwa amekifanya nchini Marekani.
Walipofika nyumbani kwa mzee Steven, wote wakateremka na kuanza kuelekea getini kisha mlinzi kuwafungulia na kuanza kuingia ndani ya eneo la nyumba hiyo. Wakaanza kuufuata mlango wa kuingilia sebuleni ambao wakaugonga na kukaribishwa ndani.
Mzee Steven na mkewe, Bi Magreth walikuwa sebuleni hapo, walipowaona wazee wenzao wanaingia, wakawakaribisha kwa furaha lakini mara walipomuona Gibson akiingia pamoja nao, wakabadilika kabisa. Nyuso za furaha ambazo walikuwa nazo zikawa zimekwishabadilika kabisa, walionekana dhahiri kutokumpenda Gibson kwa wakati huo. Hata pale Gibson alipowasalimia, hakukuwa na mtu aliyeitikia.
Wakakaa kochini na kisha kuanza kuongea na baadae kumpa ruhusa Gibson kuongea. Ila kabla hajaanza kuongea, Prisca akaitwa mahali hapo, alipomuona mume wake, akaanza kulia. Prisca alikuwa mgumu kubembelezeka, alizidi kulia zaidi na zaidi huku Gibson akiangalia chini kwa aibu.
Prisca alilia kwa muda mrefu, aliponyamaza, Gibson akaanza kuelezea kila kitu ambacho kilitokea katika maisha yake na Katie tangu kipindi kile walipokutana kazini. Gibson alikuwa mkweli, ila katika sehemu moja tu hakutaka kuwa mkweli, hakutaka kuwaeleza wazazi wake kwamba alikuwa amevunja mkataba wa ndoa kwa sababu alipewa kiasi kikubwa cha fedha, alichokisema yeye ni kwamba alivunja mkataba wa ndoa kwa sababu alijua kile alichokuwa akikifanya kutokuwa kizuri, hivyo alihitaji kurudi nyumbani kuishi na mkewe aliyekuwa akimpenda.
Alipomaliza kuelezea kila kitu akaanza kuomba msamaha. Ilikuwa ni ngumu sana kwa Prisca kumsamehe Gibson kwa sababu kile alichokuwa amemfanyia kilikuwa kitu kibaya sana kilichomuumiza moyo wake. Yalipita masaa mawili huku Gibson akiomba msamaha huku akilia kama mtoto na ndipo Prisca akaamua kumsamehe tena huku msaada wa wazazi wao ukiwa umesaidia kwa asilimia kubwa.
Baada ya hapo, Gibson akaamua kuishi na mke wake, Prisca kwa amani, hakutaka kusikia kitu chochote kutoka kwa mwanamke Katie. Moyoni mwake hakujua kabisa, hakujua kwamba alikuwa amemjeruhi sana Katie, na hivyo muda si mrefu kuanzia hapo angetaka kulipiza kiasi kwa kile kilichotokea. Huko Marekani, Katie alikuwa amebadilika, alikuwa kama mbogo aliyejeruhiwa huku akimtafuta mtu aliyemjeruhi.
Baada ya hapo, maisha yataanza kubadilika, huzuni itaingia, hasira za Katie zikabadilisha kila kitu, furaha ikawa huzuni na majonzi. Kwa Gibson hilo wala hakulitambua, alikuwa akiendelea kuishi na Prisca huku akijua kwamba yeye na Katie yalikuwa yamekwisha, kumbe ilikuwa tofauti kabisa kwani ndio kwanza mambo yalikuwa yakianza tena ngoma ikiwa mbichi kabisa...na kama gazeti, ndio kwanza ulikuwa umeanza ukurasa wa kwanza.

Je nini kitaendelea?
Je Katie atafanya nini kudhirisha hasira zake?
Je maisha yataendelea kuwa ya furaha kwa Gibson na mkewe, Prisca?
Itaendelea  kesho saa nne usiku.
imedhaminiwa na dick sound mnyama,mac auto accessories,zannel bongo ladies wear na f
acebook take away watengenezaji wa chips tamu kinondoni.

No comments:

Post a Comment