hk CONTACTS

hk CONTACTS

Thursday, May 16, 2013

MCHEZA FILAMU ZA NGONO SEHEMU YA 6.





Maisha hayakuwa ya shida tena, umasikini ambao alikuwa ameupitia pamoja na Gibson ukaonekana kutokujirudia tena katika maisha yao. Kwa wakati huo kila kitu kilionekana kubadilika kabisa. Walikuwa na fedha za kutosha, walijenga nyumba ya kifahari huku wakiwa na magari mawili ya kifahari.
Hawakuishia hapo, pia walikuwa na miladi mbalimbali ambayo ilikuwa ikiwaingizia kiasi kikubwa cha fedha. Mapenzi yao yaliendelea kama kawaida, hakukuonekana kama kulikuwa na mtu ambaye alimchoka mwenzake, walionekana kuzidi kupendana kadri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Prisca hakujua fedha zile zilitoka wapi, kila alipokuwa akiuliza, alipewa majibu ambayo wala hayakuonekana kuridhisha japokuwa baada ya muda fulani akaonekana kuyaamini. Hakujua kama fedha zile ambazo zilikuwa zikitumika kuwatengenezea maisha yao zilikuwa zikitoka kwa msichana ambaye alikuwa muigizaji mashuhuri wa filamu za ngono na ndiye ambaye kwa wakati huo alikuwa akimuibia penzi lake kutoka kwa mume wake, Gibson.
Maisha yakaendelea kusonga mbele, furaha yao ikaongezeka zaidi na zaidi, mtoto wao mpendwa, Genuine alikuwa akiwafanya kuwa karibu sana. Kutokana na fedha ambazo walikuwa nazo katika kipindi hicho, wakaanza kujulikana jambo ambalo likaanza kuwaweka katika listi ya watu mia moja ambao walikuwa na fedha nyingi ndani ya jiji la Dar es Salaam.
Maisha yaliendelea kwenda mbele mpaka pale ambapo Gibson akaelekea nchini Marekani huku akisingizia kwamba alikuwa akienda kukutana na wafadhiri wa kituo cha watoto yatima ambacho alikuwa akitarajia kukifungua jijini Dar es Salaam.
Prisca akaonekana kuridhika, katika maisha yake alikuwa akiwajali sana watoto yatima, aliwapenda kupita kawaida kwani alijua fika kwamba walikuwa wakiishi katika mazingira magumu na ya tabu kupita kawaida.
Akampa baraka zote mume wake kwamba aende na arudi salama ndani ya nchi ya Tanzania ili waendelee na maisha yao kama kawaida. Moyoni hakujua, hakujua kwamba mume wake alikuwa akienda kukutana na saplaizi ambayo ilionekana kubadilisha kila kitu katika maisha yao.
Wiki ya kwanza ikakatika, japokuwa alikuwa ameahidiana na mumewe kwamba wangewasiliana lakini haikuwa hivyo, Gibson akaonekana kuwa kimya sana. Hakukuwa na mawasiliano ambayo yalikuwa yakiendelea, kila alipokuwa akitafutwa, hakuwa akipatikana.
Baada wiki mbili kupita hapo ndipo alipokutana na taarifa ambayo ilikuwa imemchanganya kupita kiasi. Mwanamke ambaye wala hakuwa akifahamiana nae akamfuata nyumbani pale na kisha kumuonyesha picha ambazo zilikuwa zikimuonyesha Gibson akiwa ndani ya suti huku pembeni yake kukiwa na msichana ambaye alivalia shela.
Kwa jinsi picha ile ilivyokuwa ikionekana, wala hakukuwa na kitu cha kujiuliza kama pale kulikuwa na tukio gani ambalo lilikuwa likiendelea, lilionekana kuwa ni tukio la harusi kati ya watu hao wawili.
Prisca akajihisi akikosa nguvu, miguu ikaanza kumlegea na kujikuta akikaa kochini. Hakuweza kuiamini picha ile, akahitaji picha nyingine zaidi na zaidi, akaonyeshewa zaidi ya picha ishirini jambo ambalo lilimfanya kuumia zaidi.
“Mungu wangu! Gibson” Prisca aliita huku akiziweka zile picha mezani.
Tayari akaonekana kuchanganyikiwa, hakuonekana kuamini kile ambacho alikuwa amekiona kwa wakati ule. Machozi yakaanza kumtoka, hapo ndipo alipogundua sababu ambayo ilimpelekea Gibson kutokuwasiliana nae kwa kipindi kirefu tangu aelekee nchini Marekani.
“Umezitoa wapi hizi picha?” Prisca aliuliza huku akionekana kama mtu aliyechanganyikiwa.
“Kwenye mtandao. Hivi kwanza unamjua huyo mwanamke?” Mwanamke yule aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Fatuma aliuliza.
“Hapana”
“Pole sana shoga yangu. Mwanamke huyu ni mcheza fiamu za picha za ngono nchini Marekani” Fatuma alimwambia Prisca maneno ambayo yakaonekana kumshtua zaidi.
Prisca akaonekana kuchanganyikiwa zaidi, akashindwa kuvumilia kukaa mahali pale, alichokifanya kwa wakati huo ni kuondoka kuelekea chumbani huku akiwa na baadhi ya zile picha. Akajifungia na kuanza kulia, alilia kwa uchungu, hakuamini kama kweli Gibson angeweza kufanya kitu kama kile, kufunga ndoa na mwanamke wa kizungu.
Kilio chake hakikuweza kumsaidia chochote kile, aliendelea kulia zaidi na zaidi lakini ukweli bado ukabaki kuwa pale pale kwamba Gibson alikuwa amefunga ndoa na mwanamke wa kizungu ambaye alikuwa mcheza filamu za ngono, Katie.
Siku hiyo ndio ilikuwa siku ambayo ilijaa maumivu kuliko siku zote katika maisha yake. Akatoka chumbani na moja kwa moja kuelekea katika sehemu ya kuegesha magari na kuchukua gari moja aina ya Verosa, akamuweka Genuine kwenye kiti kingine na kisha kuwasha gari na kuondoka mahali hapo.
Akili yake kwa wakati huo ilikuwa ikimwambia afanye kitu kimoja tu, aondoke na kuelekea nyumbani kwa wazazi wake ambako huko angewaambia kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea na kuwaoyesha zile picha na kuwa kama ushahidi kwake.
Alipofika, akamchukua Genuine na kuanza kuingia ndani ya nyumba yao. Alipogonganisha macho yake na wazazi wake, akaanza kulia, kila kitu kikaanza kujirudia ndani ya kichwa chake.
“Kuna nini tena?” Mzee Steven alimuuliza binti yake.
Prisca hakutoa jibu la swali lile, akabaki akilia zaidi na zaidi. Katika kipindi hicho alijiona kutokuwa na nguvu za kuongea hata mara moja, alikuwa akijiskia kulia zaidi na zaidi tena kwa uchungu mkubwa.
“Prisca. Kuna nini kimetokea?” Mama yake, Bi Magreth aliuliza.
Prisca hakutoa jibu lolote lile, alichokifanya kwa wakati huo ni kuwaonyeshea wazazi wake picha zile ambazo alikuwa ameletewa na Fatuma. Wazazi wake wakazichukua na kuanza kuangalia picha moja baada ya nyingine.
“Mmmh!” Mzee Steven alisikika akiguna.
“Hii inawezekana kweli” Bi Magreth aliuliza huku akiziangalia vizuri picha zile.
Hakukuwa na mtu ambaye alikuwa akiamini kile ambacho alikuwa akikiona katika picha zile, waliziona kuwa kama picha za kutengenezwa ambazo mtu yeyote mwenye ujuzi wa kuzitengeneza angeweza kuzitengeneza.
Chini ya zile picha kulikuwa na jina la mtandao ambao picha zile zilikuwa zimechukuliwa jambo ambalo likamfanya mzee Steven kuchukua laptop yake, akaiunganisha na internet na kisha kuanza kuufungua mtandao ule.
Picha ambazo alikuwa akiziona katika mtandao ule zilikuwa ni picha zile zile ambazo walikuwa nazo mikononi na huku nyingine zikionekana kuwa mbaya zaidi ambazo zilidhihirisha kwamba watu wale walionekana kuwa mume na mke ambao walikuwa wameingia katika ndoa.
“Hivi inawezekana kwa Gibson kufanya vitu kama hivi?” Mzee Steven aliuliza huku akionekana kushangaa.
“Inawezekana na ndio maana amefanya hayo” Bi Magreth alijibu.
Kitu walichokifanya mahali hapo ni kuondoka na kuelekea nyumbani kwa mzee Lyimo ambaye alikuwa baba wa Gibson. Kwa kutumia usafiri wa gari lao, walitumia muda wa dakika thelathini wakawa wamekwishafika, wakateremka na kuanza kuelekea katika nyumba hiyo.
Muda wote huo Prisca alikuwa akiendelea kulia, bado mawazo yake yalikuwa kwa mume wake ambaye aliamua kufanya jambo lililomshtua kupita kawaida. Hamu ya kuwa ndani ya ndoa ikanekana kuanza kumtoka moyoni, hakutamani kurudi nyumbani kabisa.
“Mmmh! Inawezekana kweli kwa Gibson kufanya haya?” Mzee Lyimo aliuliza huku akionekana kushtuka kupita kawaida.
Tayari picha zile zikaonekana kumshtua kupita kawaida, hakuamini kama mtoto wake, Gibson alikuwa ameamua kuoa nchini Marekani na wakati alikuwa na mke pamoja na mtoto mdogo ambaye alikuwa na miezi kumi tu.
“Mmmh!” Mama yake Gibson, Bi Yustina aliguna.
Kila mmoja akaonekana kutokuelewa sababu ambazo zilimfanya Gibson kuamua kufanya uamuzi ule ambao ulionekana kumuumiza kila mtu aliyeziangalia picha zile. Prisca bado alikuwa akiendelea kulia kupita kawaida, moyo wake ukaanza kupatwa na majeraha ya mapenzi, mtu ambaye alikuwa akimuamini ndiye ambaye alikuwa amekuja kumuumiza.
“Inaniuma sana” Prisca aliwaambia huku akiendelea kulia.
“Pole sana Prisca”
“Sijaumia kwa yeye kuoa mwanamke mwingine tu bali nimeumia pia kwa aina ya mwanamke aliyemuoa” Prisca aisema.
“Eeeeh! Kwani unamjua?”
“Hapana”
“Sasa ni mwanamke wa aina gani?”
“Mcheza filamu za utupu”
“Unasemaje?” Wazazi wote wanne walisema kwa pamoja.
“Ndio. Ni mcheza filamu mzuri wa utupu duniani” Prisca aliwaambia.
Maneno hayo ndio ambayo yalionekana kuwachanganya zaidi na zaidi, wakaona kwamba kijana wao tayari alikuwa amepotea njia kwa uamuzi ule ambao alikuwa ameufanya. Taarifa kwamba msichana ambaye alikuwa amemuoa alikuwa mcheza filamu za ngono ilionekana kuwaumiza na kuwakasirisha kupita kawaida.
Walichokijua ni kwamba kule alipokuwa akifanya kazi Gibson, mbugani ndipo ambapo kulikuwa na uwezekano wa kukutana na mwanamke yule, walichokitaka kwa wakati huo ni kuwasiliana na mtu yeyote kutoka katika kampuni ile aliyokuwa akifanyia kazi kwa ajili ya kutaka kuufahamu ukweli.
“Nina namba ya rafiki wake wa karibu, Richard” Prisca alisema.
Hapo ndipo mawasiliano na Richard yalipoanza. Kitu ambacho alitakiwa kukifanya Richard ni kutoka Morogoro na kuja jijini Dar es Salaaam kwa kutumia usafiri wa ndege na gharama zote zilikuwa juu ya Prisca.
Ndani ya masaa kadhaa, Richard alikuwa katika nyumba hiyo ya mzee Lyimo. Kitu cha kwanza walichokifanya ni kumkabidhi Richard picha zile na kuanza kuziangalia. Richard akaonekana kushtuka, hakuamini kile ambacho alikuwa akikiona kwa wakati ule.
“Umeshtuka nini?” Mzee Lyimo alimuuliza.
“Kuona picha hizi” Richard alijibu.
“Yaani unajifanya kama haujui chochote kile”
“Yeah! Sikujua kama angefanya kitu hiki” Richard aliwaambia.
“Kwa hiyo ulikuwa ukijua kwamba ana mwanamke?”
“Hapana. Ila nilijua kwamba anakwenda nchini Marekani kwa sababu aliniaga” Richard alisema.
“Alipokuaga alikwambia nini?”
“Kwamba anakwenda kukutana na wadhamini wa kituo cha watoto yatima ambacho anataka kuanzisha” Richard alidanganya.
“Kwa hiyo haujui chochote kuhusu mwanamke huyo?”
“Sijui” Richard alijibu.
“Hapana. Kuna kitu unafahamu tu. Naomba utuambie ili tujue pa kuanzia. Unajua limekwishakuwa suala kubwa sana hili” Mzee Lyimo alimwambia Richard.
Richard hakutaka kutoa siri ya kitu ambacho kilikuwa kinaendelea. Alikuwa akikataa kuzungumza kitu chochote mpaka pale alipobanwa sana na ndipo akaanza kuelezea kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea katika kipindi cha nyuma. 
Prisca akaonekana kushtuka, hakuamini kile ambacho alikuwa amekisikia kutoka kwa Richard, hakujua kama Richard nae alikuwa akifahamu kila kitu japokuwa alikuwa mtu wake wa karibu kuliko marafiki wote wa Gibson.
“Kwa hiyo ukanisaliti? Ukawa unafahamu kila kitu ila haukutaka kuniambia?” Prisca alimuuliza Richard kwa sauti ya ukali.
“Nilihofia. Nilichokuwa nikitaka kukiona ni kuona kwamba Gibson anafanikiwa na kutoka kwenye maisha aliyokuwa anaishi. Niliamini kama angefanikiwa, hata mimi rafiki yake wa karibu ningefanikiwa pia. Na hiyo ndivyo ilivyokuwa” Richard alimwambia.
“Unamaanisha hata hizi fedha zote alizokuwa akizipata Richard zilitoka kwa mwanamke huyu?” Mzee Lyimo aliuliza.
“Ndio. Hebu jifikirieni hapo, kama ningeamua kumwambia Prisca juu ya hili, unafikiri hizi fedha wangezipata? Unafikiri Prisca angekuwa muelewa. Niliiangalia hali yao, ilikuwa hali mbaya, Prisca alikuwa mjauzito ambaye alikuwa akihitaji kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya matunzo. Kitendo cha msichana Katie kuja katika maisha ya Gibson niliona kuwa kama muujiza ambao wala haukutakiwa kuachwa kutokea. Na kweli, baada ya kumkubali Katie kisiri, mafanikio yakaja. Najua kwa kufanya hivyo nimekuumiza sana Prisca ila jua nilifanya hivyo kwa sababu sikutaka uishi maisha ya tabu mara utakapojifungua. Mshahara wa Gibson haukuwa ukitosheleza” Richard alimwambia Prisca.
Wote wakaanza kumuelewa Richard, maneno ambayo alikuwa ameyaongea yakapenya masikioni mwao na kutulia katika akili yao. Ni kweli alionekana kuwa msaada mkubwa sana kwa Prisca kwani kama angeamua kusema ukweli, Prisca angekuwa kwenye hali mbaya katika kipindi kile cha ujauzito.
“Kwa hiyo haukufahamu kama huyu binti alikuwa mcheza filamu za ngono?” Mzee Steven aliuliza.
“Sikufahamu kabisa na ninadhani kwa sababu mimi si mpenzi wa filamu hizo” Richard alijibu.
“Shukrani sana. Umeamua kuwa mkweli. Sasa tuambie kwamba hakukwambia kama alikuwa anaenda kufunga ndoa na msichana huyu?” Mzee Lyimo aliuliza.
“Hakuniambia kabisa. Kitu ambacho aliniambia ni kwamba alikuwa ameandaliwa saplaizi na mwanamke huyo, nadhani harusi ndio ilikuwa ni saplaizi yenyewe. Nina uhakika kwamba Gibson ameoa huku akiwa hataki kuoa. Naamini hilo” Richard aliwaambia
“Unawasiliana nae?”
“Hapana. Nimejaribu kumuandikia barua pepe zaidi ya tatu, naona kimya” Richad alijibu.
“Dah! Sasa ataweza kurudi nchini Tanzania?”
“Ataweza. Gibson anachokiangalia kwa mwanamke yule ni fedha tu, hakuna kingine cha zaidi. Mitego yake yote ameiweka katika fedha tu kwani anajua kwamba mwanamke yule ana fedha nyingi” Richard aliwaambia.
Waliendelea kumuuliza maswali mengi na Richard alikuwa akijibu kwa ufasaha sana bila kusema kwamba yeye ndiye alikuwa amemshinikiza Gibson kutembea na Katie. 
Maisha yakaendelea zaidi na zaidi, kila siku Prisca alikuwa mwanamke mwenye huzuni, japokuwa alikuwa na fedha za kutosha lakini fedha hazikuwa na thamani kwake, thamani kubwa ilikuwa ni Gibson ambaye alikuwa na mapenzi yake ya dhati moyoni mwake.

Je nini kitaendelea?
Je wazazi wa pande zote mbili wataamua nini?
Je maisha ya Gibson yatakuwaje nchini Marekani?
Je ndoa yao itadumu?
Hapa ndipo hadithi inapoanza rasmi.
Itaendelea saa nne usiku.

igizo hili limedhaminiwa na DICK SOUND MNYAMA,ZANEL BONGO LADIES WEAR,MAC AUTO ACCESSSORIES na FACE BOOK TAKE AWAY Ywauzaji wa chips TAM TAM kinondoni.

contact kwa udhamini 0786435543.

No comments:

Post a Comment