hk CONTACTS

hk CONTACTS

Tuesday, May 28, 2013

MCHEZA FILAMU ZA NGONO SEHEMU YA 12

 

 

 


Kila mmoja alionekana kuchanganyikiwa, kutokumkuta mtu yeyote ndani ya chumba kile kuliwachanganya zaidi. Gibson hakuonekana kuamini kile ambacho alikuwa akikiona, hakuamini kama mke wake, Prisca pamoja na mtoto wake, Genuine hakuwa ndani ya chumba kile. Kila mmoja alikuwa akijiuliza mahali ambapo walikuwepo watu hao lakini hakukuwa na mtu ambaye alikuwa na jibu.
Kitu walichokifanya ambacho kilikuwa ni cha haraka sana ni kuwasiliana na polisi na kisha kuwaelezea kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea. Ni ndani ya dakika kumi, mapolisi wa kituo cha Masaki wakafika mahali hapo huku wakiongozana na polisi wa kituo cha Oysterbay. 
Dokta akaanza kuelezea kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea hospitalini hapo kuhusiana na wazungu hao ambao walikuwa wamefika mahali hapo kama madaktari ambao walifika mahali hapo kwa ajili ya kutoa chanjo kwa watoto wadogo walio chini ya miaka mitano.
“Unasema walitoka wapi?” Gibson aliuliza.
“Nchini Marekani” Dokta alijibu.
Tayari Gibson akaonekana kuwa na wasiwasi mwingi mahali hapo, kichwa chake kikawa kama kimekwishahisi kitu fulani ambacho kilikuwa kimeendelea mahali hapo. Gibson akaondoka na kwenda kukaa pembeni kabisa ya polisi wale huku akionekana kuwa mwingi wa mawazo.
“Vipi?” Dokta alimuuliza mara baada ya kumuona akiwa ameelekea kule pembeni.
“Mke wangu na mtoto wangu”
“Usijali. Tumekwishatoa taarifa polisi, wanalifanyia kazi” Dokta alimwambia Gibson.
Polisi hawakutaka kulala, mtu ambaye alikuwa akilalamika kwamba mke wake na mtoto wake walikuwa wametekwa na watu kutoka nchini Marekani na ambao walijifanya kama madaktari walikuwa wakimfahamu sana. Gibson alikuwa ni tajiri mkubwa nchini Tanzania ambaye alikuwa akisaidia watu mbalimbali nchini hasa wale ambao walikuwa na matatizo mbalimbali.
Ni ndani ya dakika arobaini, waandishi wa habari wakafika mahali hapo na kuanza kupewa maelezo juu ya kile ambacho kilikuwa kimetokea. Muda wote Gibson hakuwa muongeaji, alikuwa kimya huku akionekana kuwa mwingi wa mawazo.
“Ni Katie. Huyu atakuwa Katie tu” Gibson alijisemea.
Mawasiliano yakaanza kufanyika, tayari polisi walikwishajua kwamba watekaji hao bado wangekuwa ndani ya jiji la Dar es Salaam tu. Simu zikaanza kupigwa sehemu mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha ulinzi huku aina ya gari lile ambalo walikuwa wameondoka nalo likiwa linatolewa taarifa kwa kila aliyeambiwa japokuwa namba zake hawakuwa wakizifahamu.
Walichokiona kwa wakati huo, walijua fika kwamba watu hao walikuwa na uwezekano wa kuondoka kuelekea Bagamoyo, Barabara ya Morogoro au ile ya kwenda Mtwara. Kitu walichoona kuwa cha maana ni kuwasiliana na polisi wote ambao walikuwa katika sehemu hizo na kuwaambia kwamba ulinzi na upekuzi wa magari ulikuwa ukihitajika kufanyika tena kwa haraka sana.
Vyombo vya habari hasa televisheni na redio vikaanza kutangaza kile ambacho kilikuwa kimetokea, kila mtu akaonekana kushangaa, taarifa ile ilionekana kuwashtua kupita kawaida. Kila mtu akalaani kitendo kile ambacho kilikuwa kimetokea, utekaji ulionekana kuwa kitu kigeni sana kutokea nchini Tanzania.
“Watekaji ni lazima wakamatwe na mateka ni lazima wapatikane wakiwa hai” Kamanda mkuu wa jeshi la polisi, Oswald aliwaambia waandishi wa habari huku mapolisi wakiwa wamekwishaanza kazi yao.
****

Taarifa ile ilikuwa ikiendelea kusambazwa kama kawaida na ilivuma kwa kasi hata zaidi ya upepo. Kila mtu ambaye alikuwa akisikia alionekana kutokuelewa ni kitu gani ambacho kilikuwa kimetokea mpaka Prisca na mtoto wake kutekwa manyara.
Polisi wakaanza kuzunguka ndani ya jiji la Dar es Salaam huku lengo lao likiwa ni kulitafuta gari lile ambalo lilikuwa linaendeshwa na watekaji wale. Kila kona, polisi walikuwa wakizunguka zunguka, watu ambao walikuwa wakisafiri kwa kutumia ndege, safari zilikuwa zimesimamishwa kwa muda, msako ulikuwa ukiendelea kila kona.
Kwa wakati huo, Gibson pamoja na dokta mkuu wa hospitali ya Masaki, dokta Philip walikuwa wamekwishafikishwa katika kituo cha polisi kwa ajili ya maelezo zaidi. Kila mmoja alikuwa akitoa maelezo yake juu ya kila kitu ambacho kilikuwa kimetokea.
“Ina maana hamna uhakika kwamba watu hao walikuwa madaktari?” Manase ambaye alikuwa polisi aliyehusika zaidi kwenye kuhoji watu alimuuliza dokta Philip.
“Sikuwa na uhakika lakini kila nilipoona vibari vyote walivyokuwa navyo, niliridhika nao na wala sikutaka kuhoji maswali zaidi” Dokta Philip alijibu.
“Kwa hiyo walikuwa na vibali vyote?”
“Ndio”
Manase hakutaka kuendelea kubaki ndani ya chumba kile, akawaacha na kisha kuelekea nje ambako huko akaanza kuongea na polisi wengine, simu zikaanza kupigwa sehemu mbalimbali na kisha kurudi tena ndani ya chumba kile.
Hadi kufikia wakati huo, hali ilionekana kuwachanganya kupita kawaida. Ni kweli walikuwa na uhakika kwamba watu wale hawakuwa madaktari lakini walivipata wapi vibali ambavyo viliwaonyesha kwamba wao walikuwa madaktari?
Kila swali ambalo walikuwa wakijiuliza lilionekana kuwachanganya kupita kawaida, kwao, watu hao wakaonekana kujiandaa kupita kawaida katika kufanya kila kitu ambacho walikuwa wamepanga kukifanya kwa wakati huo.
“Unahisi kitu chochote kile?” Manase alimuuliza Gibson.
“Ndio”
“Kitu gani?”
“Kuna mtu amehusika katika tukio hili”
“Mtu gani?”
“Kuna mwanamke mmoja amehusika”
“Mwanamke yupi?”
“Katie”
“Ndiye nani huyo?”
“Mcheza filamu za ngono aishiye nchini Marekani”
Manase na dokta Phillip wakaonekana kushtuka, jibu ambalo alilitoa Gibson likaonekana kuwashangaza sana. Hawakujua ni kwa nini Gibson aliwaamba maneno yale, hawakujua kama Gibson alikuwa na uhakika juu ya kile ambacho alikuwa amekisema au la.
“Unatuchanganya. Ndiye nani huyo?” Manase aliendelea kuuliza.
“Mcheza filamu za ngono” Gibson alijibu.
Hapo ndipo Gibson alipoanza kuelezea kila kitu kilichotokea katika maisha yake huku akizungumzia kwa undani kila kitu ambacho alikuwa amekifanya pamoja na Katie. Kila mmoja alikuwa makini akimsikiliza, mpaka anamaliza, kila mmoja alikuwa na uhakika kwamba Katie alikuwa amehusika katika mchezo mzima.
“Amehusika katika hili” Manase alimwambia Gibson.
Manase akatoka ndaniya chumba kile na kisha kuanza kuongea na wenzake kuhusiana na kila kitu ambacho alikuwa ameambiwa na Gibson. Taarifa zikaanza kutolewa sehemu mbalimbali ila kitu kikubwa ambacho kilikuwa kikihitajika kwa wakati huo ilikuwa ni kuhakikisha kwamba watekaji wale wanakamatwa na hatimae kumtaja mhusika aliyewatuma kufanya utekaji ule.
“Kuna tetesi zozote?”
“Ndio. Watu wa Chalinze walisema kwamba waliliona gari hilo likipita kwa kasi”
“Kuelekea wapi?”
“Kama si Kilimanjaro, basi itakuwa Tanga”
“Sawa sawa. Wapigieni simu polisi wa Segera na kuwaambia kwamba inawapasa kuangalia kwa makini magari yote yatakayopita huku sisi tukianza safari kwenda huko” Manase aliwaambia na kisha kutoka nje ya ofisi ile pamoja na Gibson na dokta Manase na kisha kuanza kuelekea Segera ambako walijua fika kwamba watekaji wale wasingeweza kuvuka salama bila kukamatwa.
“Chochote kitakachotokea kwa familia yangu. Nitawaua wote waliohusika” Gibson alisema huku akionekana kuwa na hasira.
****
Mara baada ya kutoka katika hospitali ya Masaki moja kwa moja safari ya kuelekea Tanga ikaanza huku wakiwa wamekwishajikamilisha kwa kila kitu. Andrew ambaye alikuwa katika usukani akiliendesha gari lile wala hakutaka wachukue muda mwingi kuchelewa njiani, kila alipoona kwamba hakukuwa na magari mengi barabarani, alikuwa akiendesha kwa mwendo wa kasi.
Prisca bado alikuwa amelala usingizi mzito huku mtoto wake, Genuine akiwa analia kupita kawaida kiasi ambacho akaanza kuonekana kuwa kero kwa watekaji wote ambao walikuwa ndani ya gari lile. Kadri Genuine alivyokuwa akizidi kulia na ndivyo ambavyo kelele zile zilionekana kuwa kero zaidi.
Hawakujua ni kitu gani ambacho walikuwa wakitakiwa kukifanya kwa wakati huo, vichwani mwao kulikuwa kukifikiriwa vitu viwili tu, ilikuwa ni lazima wamtupe mtoto huyo barabarani au kama walikuwa wakitaka kwenda nae basi ilikuwa ni lazima kufanya kitu ambacho kingemfanya mtoto yule kutokulia kwa sauti kubwa kama ilivyokuwa.
“What should we do? (Tunatakiwa tufanye nini sasa?)” Filbert aliuliza.
“Open the window (Fungua dirisha)” Reuben alimwambia Filbert.
“What for? (Ili iweje?)” Filbert aliuliza huku akionekana kushtuka.
“I want to do something (Nataka kufanya kitu)” Reuben alimwambia Filbert.
“This is crazy Reuben, dont dare to do what you want to do (Huu ni upuuzi Reuben, usithubutu kufanya hicho unachotaka kukifanya)” Filbert alimwambia Reuben.
“I have to do this Fil. If I ain’t do this, then, we are going to die (Inanibidi nifanye hiki Fil. Kama sitofanya hivi, tunakwenda kufa)” Reuben alimwambia Filbert.
Mtafaruku bado ulikuwa ukiendelea ndani ya gari huku Andrew akiwa bize kuendesha gari kwa kasi. Kitu ambacho alikuwa akikitaka Reuben kilikuwa ni kumtupa mtoto Genuine dirishani huku gari likiwa kwenye mwendo ule wa kasi lakini Filbert hakutaka kuona kitu hicho kikitokea. 
Walikuwa wamekwishafika Kimara, sehemu ambayo magari mengi yalikuwa barabarani huku hata idadi kubwa ya watu ikiwa pembezoni mwa barabara. Kitu alichokuwa akikitaka Filbert ni kumtupa Genuine katika eneo ambalo halikuwa na wakazi wengi kwani kama wangefanya vile mahali pale basi ilikuwa ni lazima kugundulika tu.
Safari ilikuwa ikiendelea kama kawaida, hakukuwa na mtu yeyote ambaye alikuwa akilitilia mashaka gari lile ambali bado lilikuwa likiendelea na safari ya kuelekea Tanga. Kutokana na mwendo wao kuwa mkali, walichukua dakika arobaini wakawa wamekwishafika Chalinze.
“Twende kulia” Reuben alimwambia Andrew ambaye akakata kulia. Ramani ambayo walikuwa nayo mikononi mwao ndio ambayo ilikuwa ikiwaongoza katika kila njia ambayo walikuwa wakienda kwa wakati huo. Lengo lao kubwa kwa wakati huo lilikuwa ni kufika Tanga ambapo huko wangeonganisha mpaka Mombasa na kuelekea Nairobi na kisha kuchukua ndege na kurudi nchini Marekani hasa mara baada ya kukamilisha kumuua Prisca.
Walitembea na gari lao kwa muda wa dakika thelathini, wakaanza kufika katika maeneo mengi ambayo hayakuwa na makazi, maeneo ambayo yalikuwa na miti mingi sehemu zilizoonekana kuwa kama pori. Hapo ndipo makubaliano yale yakafikiwa muafaka, walitakiwa kumtupa Genuine kupitia dirishani huku gari likiwa katika mwendo ule ule wa kasi.
Huku wakiwa wamekwishakubaliana kitu cha kufanya, ghafla Prisca akaamka kutoka katika usingizi na kuanza kushangaa mahali ambapo alipokuwa. Fahamu zilivyomjia vizuri, akaonekana kukumbuka kila kitu.
Kitu cha kwanza akaanza kumtafuta mtoto wake, tayari alikuwa katika mikono ya Reuben ambaye alikuwa akijiandaa kumtupa nje Genuine kupitia katika dirisha lile huku Filbert akiwa amekwishafungua dirisha.
Hata kabla Prisca hakuongea kitu chochote kile, Reuben alikifanya kitu kimoja tu, akamtupa Genuine nje kupitia dirisha huku gari likiwa katika mwendo mkali wa kilometa 120 kwa saa. Kilichosikika ni sauti ya Genuine tu ambaye akajigonga katika miti kadhaa, damu zikatapakaa katika kila mti aliojiginga na kuwa mwisho wake.
Lilikuwa ni tukio kubwa na baya katika macho ya Prisca, hakuamini kile ambacho alikuwa amekiona kwa wakati ule. Akapiga uy owe mmoja tu, akajikuta akipoteza fahamu, tukio ambalo alikuwa amelishuhudia kutupwa kwa mtoto wake lilionekana kumshtua, kumuumiza kupita kawaida.
Hakukuwa na mtu yeyote ambaye alikuonekana kujali, kitu ambacho walikuwa wakikitaka mahali hapo ni kufika Tanga ambapo wangeonganisha mpaka Mombasa, ila kabla ya kufika Mombasa, ilibidi wamuue Prisca na kisha kuendelea na safari ya kuingia Mombasa.
“Kuna tatizo mbele yetu” Andrew aliwaambia huku wakiwa wamekaribia kufika Segera, njia panda ya kuendea Kilimanjaro na Tanga.
“Kuna nini?”
“Kuna magari mengi yanaonekana kusimamishwa, nafikiri kuna kitu kinaendelea” Filbert alijibu.
“Tumia mpango B” Reuben alimwambia Andrew huku akiangalia ramani aliyokuwa ameishika.
“Usijali. Nimekusikia kiongozi” Andrew aliitikia.
****
Mpango B ukafanyika mahali hapo, Andrew akakata kona kulia na kuingia kichakani. Mwendo ulikuwa ni wa kasi sana, katika kipindi hicho tayari walikuwa wamekwishashikwa na wasiwasi kwamba polisi walikuwa wamekwishagundua na hivyo walikuwa katika kila njia kuhakikisha wanakamatwa.
Bado Andrew alikuwa akiendesha gari kwa kasi, katika kipindi hicho walidhamiria kuingia mkoani Tanga ambako wangeanza kuelekea Zigaya ambako wala hakukuwa mbali sana kuingia Mombasa nchini Kenya.
Kila mtu aklini mwake alikuwa akifikiria lake kwa wakati huo, ni kweli kwamba walikuwa wakitamani sana kufika nchini Kenya ambako huko wangechukua ndege na kuelekea nchini Marekani lakini uwepo wa Prisca ndani ya gari uliwafanya kuchanganyikiwa.
Lengo kubwa hasa ambalo lilikuwa limewaleta nchini Tanzania lilikuwa ni kumuua Prisca lakini cha kushangaza, mpaka muda huo hawakuwa wamekamilisha kile kilichokuwa kimewaleta nchini Tanzania japokuwa Prisca walikuwa nae.
Safari ilikuwa ikiendelea zaidi huku ramani ambayo walikuwa nayo ndio ambayo ilikuwa ikiwasaidia katika kuwaongoza kule ambako walikuwa wakiendelea kwenda mbele. Kwanza kitu ambacho walikuwa wakikitaka kwa wakati huo kilikuwa ni kuingia Tanga mjini ambako wangeongeza mafuta kwenye gari lao na kisha kuendelea na safari yao kama kawaida.
Masaa mawili yakakatika huku wakiwa bado wakitembea porini na ndipo wakaamua kuingia barabarani. Hapo, Andrew akaongeza mwendo zaidi, walijiona kuwa nyuma ya muda, walikuwa wakitaka kufika haraka iwezekanavyo ili kazi yao izidi kuwa nyepesi zaidi.
Wakaingia Tanga mjini saa sita kasoro mchana na moja kwa moja kuanza kuelekea katika kituo cha mafuta kwa ajili ya kuongeza mafuta kabla ya kuendelea na safari yao zaidi. Hakukuwa na mtu ambaye alikuwa na wasiwasi wowote ule, wakazi wengi wa Tanga hawakuonekana kulitilia umakini tangazo ambalo lilikuwa limetolewa katika vyombo mbalimbali vya habari juu ya utekaji ambao ulifanyika jijini Dar es Salaam.
“Lets make hurry (Tufanyeni haraka)” Filbert aliwaambia.
“Dont worry. We are safe in here (Usihofu. Hapa tupo salama)” Reuben alimwambia Filbert huku akionekana kutokuwa na wasiwasi wowote ule.
“There is no more peace. I have seen the news on the television about us (Hakuna amani hapa. Nimeona habari kwenye runinga kuhusu sisi)” Filbert aliwaambia.
“Thats not true. When did you learn to undrestand Swahili language? (Hiyo si kweli. Umejifunza lini lugha ya Kiswahili?)” Reuben aliuliza huku uso wake ukiwa na tabasamu.
“I saw Gibson on the television, then tell me what do you think is goin on (Nimemuona Gibson runingani, aya niambie unafikiri nini kinaendelea?)” Filbert alikuwa akijitahidi kuelezea kila kitu ambacho alikuwa amekiona kwenye televisheni lakini hakukuwa na mtu yeyote ambaye alionekana kumuamini, wote walimuona Filbert kuwa mtu muoga sana.
Kitu ambacho walikuwa wakikitaka kwa wakati huo ni kula chakula hata kabla safari yao haijaendelea zaidi na zaidi. Wakaenda hotelini na kuingia ndani, wakala chakula na kisha kuendelea na safari yao.
Muda wote huo, Prisca alikuwa amepoteza fahamu, mshtuko mkubwa ambao alikuwa amekutana nao ulikuwa ulimfanya kuwa katika usingizi mzito mpaka katika kipindi hicho. Hakukuwa na mtu ambaye alionekana kujali, kupoteza fahamu kwa Prisca kulionekana kuwa nafuu kwao kwa kuamini kwamba hakukuwa na usumbufu wowote kwa wakati huo ndani ya gari.
Wakaanza kushika barabara ya kuelekea Mombasa, daladala nyingi zilikuwepo njiani, idadi ya watu ilikuwa kubwa barabarani huku kila sehemu kukionekana kuwa na uchangamfu mkubwa. Kitu ambacho walikuwa wamekifanya kwa wakati huo, waliandaa fedha za kutosha kwa kuamini kwamba kama wangefika mpakani, wasingeruhusiwa kuvuka ila kwa kutumia dola ambazo walikuwa nazo, wala kusingekuwa na tatizo lolote lile.
Safari iliendelea mbele zaidi na zaidi, tayari walikuwa wamekamilisha asilimia themanini ya kazi ambayo walikuwa nayo na zilibakia asilimia ishirini tu, za kuingia Mombasa, kusafiri mpaka Nairobi na kisha kuchukua ndege na kurudi nchini Marekani huku wakiwa na ushindi mkubwa mioyoni mwao kitu ambacho kingekuwa furaha kubwa kwa Katie ambaye alikuwa amewatuma nchini Tanzania.
“Tufanyeni kitu kimoja” Filbert aliwaambia.
“Kitu gani?” Reuben aliuliza.
“Tumuueni huyu mwanamke kabla hatujaingia nchini Kenya. Yaani namaanisha kabla hatujafika mpakani”
“Wazo lako zuri. Nafikiri umeona kwamba anaweza kutuletea matatizo hapo mpakani”
“Hilo ndilo nililolifikiria” Filbert aliwaambia.
Wazo ambalo lilitolewa na Filbert likaonekana kufaa sana, walichokifanya kwa wakati huo ni kukata kona na kisha kuanza kuingia porini, sehemu ambayo wangeweza kumuua Prisca huko na kisha kuendelea na safari yao ya kuelekea mpakani.
Ghafla, Prisca akarudiwa na fahamu, akabaki akimwangalia kila mtu ndani ya gari lile. Kwa mara ya kwanza hakuonekana kukumbuka kitu chochote kile ila baada ya sekunde kadhaa, akakumbuka mambo mengi, likiwepo lile la kutupwa kwa mtoto wake, Genuine.
Prisca akaanza kulia, akamvamia Reuben kwa lengo la kupambana nae kwa kile kitendo cha kumtupa mtoto wake nje ya gari na wakati gari hilo lilikuwa kwenye mwendo wa kasi. Reuben akafanikiwa kumdhibiti Prisca ambaye akalazwa kitini huku akiwa amekandamizwa na kiganya cha Reuben.
Walipofika porini zaidi, gari likasimamishwa na kisha Reuben kumtoa Prisca nje ya gari huku akiwa amemshika shingoni. Prisca alikuwa akilia kama mtoto, akili yake kwa wakati huo ilikuwa kama imechanganyikiwa, hakumpenda Reuben hata kidogo, alikuwa akimchukia kupita kawaida.
“Niachieeeeee....niachieeee” Prisca alikuwa akipiga kelele lakini Reuben hakuweza kumuachia.
Kila kitu kwa wakati huo kikaonekana kuwa na amani, mazingira yalionekana kumridhisha kila mtu. Kitendo kilichokuwa kikitakiwa kufanyika mahali hapo kilikuwa ni kumuua Prisca na kisha kuondoka kuelekea mpakani.
Alichokifanya Reuben kwa wakati huo ni kuanza kumkaba roba kali Prisca. Prisca akabaki akitoa milio ya tofauti tofauti huku akijitahidi kutaka kuitoa mikono ya Reuben shingoni mwake lakini wala hakuweza kufanikiwa hata kidogo. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo Reuben alivyomkaba zaidi na zaidi.
Ghafla, Prisca akaanza kuona kizunguzungu huku giza la mbali likianza kuonekana mbele yake. Tayari kwa wakati huo alikuwa amebakisha muda mchache sana wa kuwa hai, muda ambao wala haukuzidi hata dakika mbili. Giza lile alilolkuwa akiliona kwa mbali likaanza kumsogelea zaidi na zaidi, baada ya hapo, akayafumba macho yake huku akihisi mtoa roho akiwa amekwishamfikia kwa ajili ya kuichukua roho yake.

Je nini kitaendelea mahali hapo?
Je Prisca amekufa?
Je watekaji watakamatwa?

No comments:

Post a Comment