hk CONTACTS

hk CONTACTS

Saturday, May 25, 2013

MCHEZA FILAMU ZA NGONO SEHEMU YA 11



Gibson alikuwa amekaa ofisini mwake huku akiendelea kufanya kazi zake kama kawaida. Kwa wakati huo, akili yake alikuwa ameituliza kwa mke wake tu, hakutaka kumfikiria Katie wala kitu chochote ambacho kilikuwa kimetokea katika maisha yake pamoja na Katie. 
Alikuwa amekwishaomba msamaha kwa mke wake kwa hiyo wala hakutaka kumkasirisha tena na wala hakutaka kutembea nje ya ndoa. Moyo wake ulikuwa ukimpenda mke wake zaidi ya kitu chochote kile katika maisha yake.
Mtoto wao, Genuine alikuwa chachu kubwa ya mapenzi yao, alimpenda sana mtoto wake na kumthamini sana. Mara kwa mara alikuwa akitamani kuwa karibu nae, kila alipokuwa akimwangalia Genuine, alikuwa akiona umuhimu wa kumpenda zaidi mke wake, Prisca.
Gibson aliendelea kufanya kazi zake kama kawaida. Ilipofika saa nne asubuhi, akaanza kujisikia hali ya tofauti moyoni mwake. Moyo ukaanza kujaa majonzi huku ukiwa mzito. Hali hiyo haikuonekana kuwa ya kawaida moyoni mwake, akaacha kufanya kila kitu na kutulia.
Hali haikuonekana kubadilika, bado alikuwa akiendelea kuihisi hali ile ile. Amani moyoni mwake ikatoweka, alichokifanya kwa wakati huo ni kuichukua simu yake na kuanza kuangalia baadhi ya namba, alipoona ameridhika, akampigia simu mke wake.
“Umefikia wapi?” Gibson alimuuliza Prisca.
“Kuhusu nini mpenzi?”
“Kumpeleka mtoto hospitalini”
“Ndio najiandaa mpenzi. Nilikuwa nikimnywesha uji kwanza”
“Sawa. Nisubiri nakuja”
“Vipi kuhusu kazi?”
“Hakuna tatizo mpenzi. Moyo wangu umekuwa mzito sana kubaki ofisini, amani imenitoweka kabisa moyoni” Gibson alimwambia Prisca.
“Mmmh! Sasa tatizo nini?”
“Bado sijajua. Nisubiri nije huko huko. Nitataka kuwa karibu na familia yangu” Gibson alimwambia Prisca.
“Sawa. Nakusubiri mpenzi” Prisca alijibu na kisha kukata simu.
Gibson hakutaka kuendelea kubaki ndani ya ifisi ile, alichokifanya ni kutoka na kisha kuanza kuelekea sehemu ya magari na kuchukua gari lake na kuanza kuelekea nyumbani kwake. Hali ya moyo wake wala haikubadilika kabisa, ilikuwa vile vile. Mawazo yalikuwa yakimsonga kichwani mwake, hakujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kikitaka kutokea ambacho mpaka katika wakati huo kilikuwa kimemkosesha amani kabisa.
“Kuna nini tena? Mbona najisikia hivi moyoni?” Gibson alikuwa akijiuliza mara kwa mara lakini hakupata jibu lolote lile.
Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo hali ile ilivyozidi zaidi na zaidi, alikuwa akiendesha gari lake lakini akili yake ilikuwa ikifikiria mambo mengi kwa wakati huo. Alikuwa akizifikiria biashara zake kwa kuona kwamba labda kungekuwa na kitu kingetokea au aliona dalili fulani lakini kila alipokuwa akijzifikiria, hakuona jambo lolote lile baya.
Alifika nyumbani baada ya dakika kumi, kitu cha kwanza ni kuelekea chumbani kwake, alipokuta mke wake, akamkumbatia kwa furaha. Akaendelea kumuelezea mke wake juu ya hali ambayo alikuwa nayo moyoni, Prisca ndiye mtu pekee ambaye alikuwa akimtoa wasiwasi moyoni mwake.
“Usijali mume wangu. Kila kitu kitakuwa salama tu na wala halitotokea jambo lolote lile baya” Prisca alimwambia Gibson.
“Una uhakika?”
“Yeah! Hatutakiwi kuogopa kitu chochote kile mpenzi” Prisca alimuondoa wasiwasi Gibson.
“Ok! Twende huko hospitalini. Leo sitaki kukaa mbali nanyi kabisa. Ninyi ndio kila kitu kwangu” Gibson alimwambia Prisca.
Alipomaliza kujiandaa, Prisca na Gibson wakaanza kuelekea garini na kisha kuanza safari ya kuelekea katika hospitali hapo Masaki. Walitumia dakika chache sana wakawa wamekwishafika katika hospitali ile ambapo Prisca akaelekea kujiandikisha na kurudi benchini kwa mumewe.
“Vipi?”
“Nimejiandikisha tu”
“Kwa hiyo inabidi usubiri hapa kama wenzako?”
“Ndio”
“Sawa”
Waliendelea kukaa katika lile benchi huku wanawake wengine wakiendelea kufika mahali pale pamoja na watoto wao. Baada ya dakika thelathini, zamu ya Prisca ikafika na kuingia ndani ya chumba kile kwa ajili ya kuhudumiwa huku Gibson akimsubiria benchini.
Dakika ziliendelea kusonga mbele lakini Prisca hakutoka nje ya chumba kile jambo ambalo lilionekana kumtia wasiwasi Gibson na kuwakasirisha wanawake wengie ambao walionekana kuwa na haraka. Gibson akaendelea kuwa mvumilivu, nusu saa ya kwanza ikapita, saa moja likatimia lakini Prisca hakuweza kutoka ndani ya chumba kile.
Gibson akaonekana kushikwa na wasiwasi, hakujua ni kitu gani ambacho kilikuwa kikiendelea ndani ya chumba kile mpaka mke wake kucheleweshwa kutoka namna ile na wakati wanawake wengine walikuwa wakitumia dakika tano hadi kumi.
Gideon akasimama na kuanza kuusogelea mlango ule na kisha kutaka kuufungua, mlango ulikuwa umefungwa kwa ndani. Tayari Gibson akazidi kushikwa na wasiwasi zaidi, alicokifanya ni kuwasiliana na ofisi ya dokta mkuu ambaye akafika mahali hapo haraka sana.
Wote wakajaribu kufungua mlango lakini wala haukufunguka. Kila mmoja alibaki kuwa na maswali juu ya kitu ambacho kilikuwa kikiendelea ndani ya chumba kile. 
“Ngoja nipitie mlango wa nyuma” Dokta kuu, Kimaro alimwambia Gibson.
“Kuna mlango wa nyuma?” Gibson aliuliza.
“Ndio”
Gibson hakutaka kumuacha daktari aende peke yake, alichokifanya ni kwenda pamoja nae. Walipofika nyuma, mlango ulikuwa umefungwa lakini walipojaribu kuufungua, ulifunguka. Kila mtu akapigwa na mshangao, ndani ya chumba kile hakukuwa na mtu yeyote yule jambo ambalo lilionekana kumshtua kila mtu.
“Hawapo. Mungu wangu! Mke wangu na mtoto wangu!” Gibson alisema kwa mshtuko.
*****
Huduma za kuwahudumia watoto zilikuwa zikiendelea kama kawaida hu wakiwa wamekabidhiwa chumba ambacho kilikuwa na mlango wa nyuma ambao ulionekana kuwa kama mlango wa tahadhari. Japokuwa mlango huo ulikuwa haujafunguliwa kwa muda wa miaka mitatu lakini Reuben akahitaji mlango huo ufunguliwe.
Hakukuwa na daktari ambaye alileta ubishi wowote ule, mlango ukafunguliwa. Saa nne asubuhi, huduma ya chanjo kwa watoto ikaanza, wanawake wengi walikuwa wamewaleta watoto wao kwa ajili ya kufanyiwa chanjo. Walichokifanya Reuben, Filbert na Andrew ni kuwaandikisha wanawake ambao walikuwa wakiwaleta watoto wao pamoja na majina ya wanaume ambao walikuwa wamezaa nao.
Hiyo ndio ilionekana kuwa nafasi pekee ambayo ingewafanya wao kumjua mwanamke ambaye angekuja mahali hapo na kuona kwamba huyu alikuwa mke wa mtu ambaye walikuwa wakimtafuta, Gibson. Wanawake walizidi kumiminika hospitalini hapo pamoja na watoto wao ambako moja kwa moja wakajiandikisha majina yao. 
“Is she here? (Yupo hapa?)” Reuben alimuuliza Filbert ambaye alikuwa akiendelea kuandikisha majina.
“Nope. She ain’t here (Hapana. Hayupo hapa)” Filbert alijibu.
Bado wanawake walikuwa wakiendelea zaidi na zaidi kujiandikisha katika kupata huduma za watoto wao kupatiwa chanjo katika hospitali ile kutoka kwa wazungu ambao walionekana kuja kutoa msaaada bila kufahamu lengo ambalo lilikuwa limewaleta mahali pale na kujifanya kutoa huduma hiyo.
Dakika ziliendelea kwenda mbele mpaka pale ambapo Prisca alipokuja kujiandikisha. Filbert akaonekana kushtuka, hakuamini kwamba hatimae walikuwa wamempata mtu ambaye walikuwa wakimsubiria kwa kipindi kirefu. Alichokifanya ni kusimama na kuelekea ndani ya chumba kile cha tiba huku lengo lake likiwa ni kuongea na wenzake.
“She is here (Yupo hapa)” Filbert aliwaambia.
“Are you sure? (Una uhakika?)
“100% (Asilimia mia moja)”
Reuben hakuonekana kuamini, alichokifanya ni kuufungua mlango huku akijifanya kuwaangalia wanawake ambao walikuwa wamekusanyika katika mabenchi. Wanawake zaidi ya ishirini walikuwa wamekaa kwenye mabenchi yale huku mwanaume akiwa mmoja tu, Gibson.
“There she is (Yule pale)” Fibert alimwambia Reuben.
Tabasamu pana likaonekana usoni mwa Gibson, tayari alikuwa ameyaona mafanikia makubwa mbele yao, kitendo cha Prisca kufika mahali pale kilionekana kumfurahisha kupita kawaida. Alikuwa na uhakika wa asilimia mia moja kwamba yule ndiye alikuwa mke wa mtu ambaye walikuwa wakimsubiria mahali hapo kutokana na Gibson mwenyewe kuonekana pembeni yake.
Walichokifanya ni kuendelea kutoa huduma kama kawaida yao. Waliandaa kila kitu, gari ambalo walikuja nalo tayari walikuwa wamekwishalipeleka nyuma ya chumba kile ili lisiwape usumbufu wowote wakati wa kutoka katika hospitali hiyo.
Wanawake waliendelea kuingia na kutoka mpaka pale zamu ya Prisca ilipowadia. Akasimama huku akiwa amembeba mtoto wake, genuine na kuingia ndani ya chumba kile huku mume wake, Gibson akiwa amemuacha benchini.
Kitu alichokifanya Reuben wakati Prisca ameingia ndani ni kumchukua mtoto wake, Daniel na kisha kumvutisha Prisca kitambaa kilichokuwa na dawa ya usingizi, wala hazikupita hata sekunde kumi, Prisca akapitiwa na usingizi mzito.
Hakukuwa na muda wa kuchelewa mahali hapo, walichokifanya ni kumbeba Prisca pamoja na mtoto wake na kisha kuanza kuelekea nae nje ambako wakawaingiza ndani ya gari. Kila kitendo ambacho kilikuwa kikiendelea mahali hapo, hakukuwa na mtu ambaye alikuwa akikiona kutokana na lile gari kupakiwa nyumba kabisa ya chumba kile, mahali ambapo si watu wengi walikuwa wakifika mara kwa mara.
“What next? (Nini kinafuata?)” Andrew aliuliza.
“Lets get out of here (Tuondokeni mahali hapa)” Reuben aliwaambia na kisha Andrew kuwasha gari lile.
Andrew hakutaka kuendesha gari kwa mwendo wa kasi kwa kuogopa kushtukiwa, alichokifanya ni kuendesha gari kwa mwendo wa taratibu na kutoka nje ya hospitali ile huku kukiwa hakuna hata mtu mmoja ambaye alikuwa akifahamu kitu ambacho kilikuwa kikiendelea mahali pale.
Safari ambayo walikuwa wameipanga kwa wakati huo ilikuwa ni kuondoka na kuelekea Tanga ambako huko wangeumuua Prisca porini na kuunganisha safari yao kuelekea Mombasa na kisha kuelekea Nairobi ambako wangepanda ndege na kuelekea nchini Marekani huku wakiwa wamekwishakamilisha kila kitu walichokuwa wameambiwa wakamilishe nchini Tanzania.

Je nini kitaendelea?
Je Reuben na wenzake wataweza kumuua Prisca kama walivyopanga?
Je watekaji wataweza kukamatwa?
Itaendelea saa moja kamili usiku.
Usikose.

No comments:

Post a Comment