Pages

Thursday, January 9, 2014

Jackie Cliff Apewa Siku 447 Kujifunza Lugha Itumikayo Macau Kwa Ajili Ya Kesi Yake ..



Mrembo na video vixen Jackie cliff, imeripotiwa hivi karibuni kuwa mwana dada huyo atalazimika kujifunza lugha ambayo hutumika na wakazi wa jiji la Macau nchini China, ambapo ni mji aliokamatwa mwana dada huyu kutokana na kosa lake la usafirishaji wa madawa ya kulevya kwa ajili ya kufanya biashara haramu ya uuzaji wa heroin.

Mwana dada huyu hivi karibuni ilidhibitishwa kuwa amekamatwa na kilo 1.1 ya Heroin katika Airport ya mji huo wa Macau. Kutokana na kesi hiyo mwanadada huyu anatakiwa kupanda kizimbani ili aweze kujitetea kutokana na kosa hilo, ila kwa sasa uongozi wa sheria wa mji huo umeamua kumpa fursa ya muda wa mwaka mmoja na nusu ambao ni sawa na siku 447 kwa ajili ya kujifunza lugha ya Kireno, ambayo ndiyo lugha ambayo hutumika mjini humo kwa wingi na pia ndio lugha itakayotumika kuendeshea kesi ya mrembo huyo

No comments:

Post a Comment