Pages

Sunday, March 24, 2013

MOROCCO YALALA 3-1 KWA KILI TAIFA STARS


Taifa Stars 3-1 Morocco

Taifa Stars imefanya kile Watanzania walichowatuma baada ya kuwalaza Simba wa Atlas kwa mabao matatu kwa moja. Kipindi cha kwanza Stars walicheza kandanda la kuvutia na kupoteza nafasi nyingi za wazi huku Mbwana Samatta akionekana kuwa mwiba mkali kwa beki ya Morocco muda wote. Katika kipindi cha pili, Thoma Ulimwengu akitokea benchi alifunga bao la kwanza baada ya kuunganisha mpira wa kona, Dakika ya 66 ilikuwa ni Mbwana Samatta ambaye alimchambua golikipa wa Morocco na kufunga bao la pili na kuongeza bao la tatu katika ya 80. Stars iliendelea kushambulia kwa kasi huku ikigonga mwamba mara mbili. Dakika ya 90 Morocco ilipata bao la kufutia machozi na hivyo mchezo kuisha kwa 3-1.

No comments:

Post a Comment