Pages

Wednesday, May 22, 2013

MCHEZA FILAMU ZA NGONO SEHEM YA 10



 Vyombo vingi vya habari nchini Marekani vilikuwa vikitangaza kuhusiana na kuvunjika kwa ndoa kati ya mwanamke ambaye alikuwa maarufu duniani katika uigizaji wa filamu za ngono, Katie pamoja na mwanaume kutoka nchini Tanzania, Gibson.
Kila mtu ambaye aikuwa akiziangalia taarifa zile katika vyombo mbalimbali vya habari hakuonekana kushtuka sana kutokana na kufahamu kwamba kuna siku kitu kama kile kingetokea kutokana na Katie kuwa miongoni mwa watu ambao waikuwa wakiigiza filamu za ngono duniani.
Kila kitu kilionekana kubadilika sana katika maisha ya Katie, mwanaume ambaye alikuwa akimheshimu sana, Gibson kwa wakati huo hakuwa pamojanae. Katie akawa mwanamke wa kulia tu, kila siku alikuwa akijifungia chumbani kwake na kulia kupita kawaida.
Moyo wake ulikuwa ukimuuma kupita kawaida. Kuna wakati alikuwa akijuta sababu zilizompelekea kuolewa na mwaname ambaye wala hakuwa amekaa nae sana katika mahusiano huku wakati mwingine akijuta sababu ambazo zilimpelekea kutokumwambia Gibson ukweli juu ya kazi ambayo alikuwa akiifanya ya uigizaji wa filamu za ngono.
Alijua ni lazima kungekuwa na sababu moja kubwa ambayo ilimfanya Gibson kuamua kufanya uamuzi wa namna ile kwani alijua kwamba Gibson hakuwa na lengo la kumuacha kwa wakati ule kutokana na sababu kubwa ya kumruhusu kwa moyo mmoja kuendelea kuigiza filamu za ngono.
Wasiwasi ukaanza kumuingia Katie kwamba kulikuwa na mtu ambaye alikuwa nyuma ya mpango ule wote, alichokifanya kwa wakati huo ni kuanza kupeleleza. Kazi ya upelelezi ilikuwa kubwa sana kitu ambacho kikamfanya kuwaita vijana maalumu kwa ajili ya kuifanya kazi ile.
Vijana waliifanya kazi ile kwa moyo mmoja, waliangaika kila sehemu lakini mwisho wa siku hawakupata kitu. Katie akaonekana kuchanganyikiwa, alichokifanya kwa wakati huo ni kuanza kuyafuatilia maisha ya Gibson tu.
Alijua fika kwamba Gibson alikuwa akielewa kila kitu juu ya sababu ambazo zilimfanya kutaka ndoa ivunjwe kwa haraka sana, umuhimu wa kumuuliza Gibson ulikuwa ukionekana kufaa kwa asilimia zaidi ya mia moja.
Katie akaanza kugundua vitu fulani, kwanza akaanza kujiuliza juu ya siku ile ambayo Gibson alikuwa ametekwa na kisha kumwambia kwamba alikuwa amewatoroka watekaji. Swali ambalo lilikuwa kichwani mwa Katie ni kwa namna gani Gibson alikuwa ameweza kupigana na watekaji hata bila kujeruhiwa katika sehemu yoyote ya mwili wake na wakati watekaji wale walikuwa na bunduki?
Katie akaanza kuingiwa na wasiwasi, akaanza kujua kwamba kulikuwa na kitu ambacho kiliendelea na aliamini kwamba kitu hicho ndicho ambacho kilimfanya Gibson kutaka kuachana nae na kuuvunja mkataba wa ndoa ambao walikuwa wameusaini.
“There’s something (Kuna kitu)” Katie alisema.
Wazo jingine likaingia kichwani mwa Katie, akaanza kugundua kwamba kulikuwa na kitu ambacho kilikuwa kikiendelea nchini Tanzania ambacho hicho nacho kilikuwa kimechangia kwa asilimia kubwa kwa Gibson kuamua kufanya vile.
Katie akaanza kugundua kwamba kulikuwa na uwezekano Gibson alikuwa na mpenzi nchini Tanzania ambaye alikuwa ameishika akili yake kupita kawaida na ndio maana alitaka kuachana nae ili aeze kurudi nchini Tanzania na kuendelea na maisha yake.
Alichokifanya kwa wakati huo ni kuwatuma vijana wake nchini Tanzania kwa ajili ya kuufanya upelelezi ambao kwake aliuona kumletea majibu yote. Alihitaji kila kitu kifanyike huku akiwaelekeza kwamba ilikuwa ni lazima kwao kufikia katika mbuga ya Mikumi ili kupata ukweli juu ya kila kitu kuhusiana na Gibson.
“Nitawagawia kila kitu, ninachokitaka kutoka kwenu watatu ni kunipa kila kitu nitakachotaka kukifahamu” Katie aliwaambia vijana wake watatu ambao walikuwa wakijiandaa kuja nchini Tanzania.
“Sawa! Hautakiwi kuhofia kitu chochote. Kuna kingine?” Reuben aliuliza.
“Ndio! Kama anaishi na mwanamke, inatakiwa mmuue kama kisasi changu” Katie aliwaambia.
“Sawa! Kingine bosi”
“Ni hivyo tu” Katie alisema.
Alichokifanya kwa wakati huo ni kuwagawia vijana wale kiasi cha dola milioni moja kwa ajili ya kuja nchini Tanzania huku fedha nyingine akiwatumia pale ambapo wangekuwa wanazihitaji wakati watakapokuwa nchini Tanzania.
Harakati za kutafuta viza zikaanza mahali hapo, wala hawakupata tabu kutokana na kuelezea katika ubalozi wa Tanzania kwamba walikuwa wakitaka kuja nchini Tanzania kwa ajili ya kufanya utalii tu. Mara baada ya kupata viza, wakakata tiketi za ndege na siku iliyofuata kuanza safari ya kuja nchini Tanzania kufanya kile ambacho kilikuwa kikitakiwa kufanyika tu.
****
Reuben, Filbert na Andrew walikuwa ndani ya ndege ya Gulf Airlines wakielekea nchini Tanzania. Muda wote walikuwa wakiongea mambo mbalimbali ambayo walitakiwa kuyafanya nchini Tanzania, ramani kubwa ya nchi ya Tanzania ilikuwa mikononi mwao kwa kuwa walikuwa wakihitaji msaada mkubwa sana wa kufika kule walipoelekezwa bila kumuuliza mtu yeyote yule.
Ndege ilichukua masaa zaidi ya ishirini na ndipo ikaanza kutua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwl Nyerere. Walipofika hapo, hawakutaka kukaa sana, walichokifanya ni kukata tiketi ya ndege ya kuelekea Morogoro huku lengo lao likiwa ni kufika katika mbuga ya Mikumi na moja kwa moja kuelekea katika hoteli iitwayo Mikumi National Park ambako huko ndipo wangeanza kumuulizia mtu ambaye walikuwa wakimtafuta, Gibson Lyimo.
Safari ya kwenda mkoani Morogoro ikaanza kwa kutumia ndege ya Precious na baada ya saa moja kuingia mkoani Morogoro ambako wakaanza kuyafuata magari ya kuelekea katika mbuga hiyo na kisha kuanza safari. Kila mmoja akilini mwake alikuwa akifikiria lake tu, mtu ambaye walitakiwa kumuua hakuwa huyo Gibson bali mtu ambaye alitakiwa kuuawa alikuwa mwanamke ambaye alikuwa akiishi nae katika kipindi hicho.
Walipofika katika hoteli hiyo iliyokuwa mbugani, wakachukua vyumba na kutulia huku upelelezi ukifanyika chini kwa chini. Walikaa katika hoteli hiyo kwa muda wa siku mbili na ndipo walipoamua kumuulizia Gibson kupitia kwa mkurugenzi wa hoteli hiyo.
“Mnamuuizia Gibson! Huyo mtu aliacha kazi kipindi kirefu cha nyuma. Kwa sasa hivi ni miongoni mwa watu wenye fedha nyingi sana hapa nchini” Mkurugenzi wa hoteli hiyo, Massawe aliwaambia.
“Kwa hiyo hatuwezi kupafahamu anapokaa?” Reuben aliuliza.
“Anakaa Dar es Salaam. Labda kama mnataka kulipia ili mfanyakazi wangu awapelekea huko mpaka nyumbani kwake” Massawe aliwaambia.
Reuben na wenzake hawakuwa na jinsi, kitu ambacho walikuwa wakikitaka kwa wakati huo ni kumfahamu mwanamke ambaye alikuwa akiishi na Gibson na kisha kufanya kile ambacho walikuwa wameagizwa, walichokifanya ni kumlipa mkurugenzi na kisha kupewa kijana mmoja ambaye walianza safari nae ya kuelekea Dar es Salaam.
Njiani hawakukaa kimya, mara kwa mara walikuwa wakimuuliza maswali mbalimbali kijana yule ambaye walikuwa nae kama namna mojawapo ya kuchunguza zaidi na kufahamu mambo mbalimbali kuhusiana na jiji la Dar es Salaam ambalo walikuwa njiani kuelekea uko.
Walipofika Dar es Salaam, moja kwa moja wakakodi teksi mbili ambazo ziliwapeleka mpaka hotelini na kisha Reuben peke yake kutoka na kuelekea uko alipokuwa akiishi Gibson huku akiongozana na yule kijana. 
“Do you see that house? (Unaiona nyumba ile?)” Kijana yule alimuuliza Reuben huku akimuonyeshea nyumba aliyokuwa akiishi Gibson.
“Please! Stop the car (Tafadhali! Simamisha gari)” Reuben alimwambia dereva ambaye alisimamisha gari lile.
“Thank you for your help (Asante kwa msaada wako)” Reuben alimwambia kijana yule huku akimtaka dereva kuwarudisha hotelini.
“So, why dont you want to meet him? (Kwa hiyo kwa nini hautaki kuonana nae?)” Kijana yule alimuuliza Reuben.
“I wanted to know the place (Nilitaka kupafahamu)”Reuben alimwambia.
****
Mchakato bado ulikuwa ukiendelea kama kawaida, walihitaji kufanya mambo yao kwa haraka haraka hata kabla wiki haijakatika na kuwakutia ndani ya jiji la Dar es Salaam. Kitu ambacho walikuwa wakikitaka katika kipindi hicho kilikuwa ni bunduki tu.
Hawakutaka kumuua mke wa Gibson kwa kutumia silaha yoyote zaidi ya bunduki, wakaanza kuangalia uwezekano wa kupata bunduki lakini kila walivyoangalia, hawakuona dalili ya kuweza kuipata aina ya silaha hiyo.
Hawakutaka kujiuliza maswali mengi sana, wakaona kwamba hata mikono yao ilikuwa na nguvu sana kukabiliana na huyo mtu tena alikuwa mwanamke, kwao alionekana kutokuwa na usumbufu wowote ule. Wakajipanga upya, ilikuwa ni lazima utekaji ufanyike, tena kwa haraka sana.
Hawakujiuliza sana kuhusiana na usafiri ambao wangeutumia siku hiyo, teksi ya kukodi ndio ambayo ingetumika katika kufanya safari zao za huku na kule. Walichokifanya mara baada ya kuweka majadiliano ya muda mrefu, wakachukua ramani ambayo ilikuwa katika begi na kisha kuanza kuiangalia kwa makini.
Wakaanza kupanga kila kitu kwamba mara baada ya kumaliza kufanya kazi ambayo ilikuwa imewaleta nchini Tanzania basi ilikuwa ni lazima kuondoka kuelekea nchini Kenya tena kwa gari kwa kupitia njia ya Tanga, njia ambayo ingewafanya kutokea Mombasa na kisha huko kupanda ndege na kurudi nchini Marekani.
Kwao, kazi hiyo wala haikuonekana kuwa ngumu hata kidogo, waliona kwamba ingeweza kufanyika ndani ya masaa machache hata kabla ya kumtaarifu Katie na kumwambia kwamba kazi aliyokuwa amewatuma ilikuwa imefanyika, tena kwa mafanikio makubwa bila kuwa na tatizo hata moja.
Walipanga mambo mengi sana, walichokuwa wameanza kukifanya ni kuanza kwenda katika mtaa aliokuwa akiishi Gibson na kisha kuangalia mandhari yote. Hawakuona kama kungekuwa na ugumu sana, mitaani huko wala hakukuwa na kamera kama ilivyokuwa katika mitaa mingi jijini New York ambayo ilikuwa ikikaliwa na matajiri, mpaka hapo, tayari wakaiona kazi hiyo ya kumteka Prisca kuwa nyepesi sana.
Muda mwingi walikuwa wakishinda ndani ya chumba cha hoteli huku mishemishe yao ikiendelea kama kawaida, kila kitu ambacho walikuwa wakikipanga kilionekana kutokufaa, hivyo walikifuta na kuanza kupanga tena.
“I will be a doctor (Nitakuwa daktari)” Reuben aliwaambia wenzake.
“Ok! We will be your assistants (Sawa! Tutakuwa wasaidizi wako)” Filbert alimwambia Reuben.
Mpango ambao walikuwa wameufikia kwa wakati huo ilikuwa ni lazima wajifanye madaktari ambao walikuwa wametoka nchini Marekani kuja nchini Tanzania kwa ajili ya kuwatibia watoto na kuwapa chanjo ambayo ingekuwa na uwezo wa kuzuia magonjwa mbalimbali hasa katika kipindi cha ukuaji.
Wote walikuwa wamekwishajua kwamba Gibson alikuwa akiishi na mwanamke ambaye alikuwa na mtoto mdogo hivyo kama wangetumia njia hiyo ingekuwa ni rahisi kwao kumpata mwanamke huyo na kisha kutoroka nae kuelekea porini na kumuulia huko huko mbele ya safari kabla ya kuanza safari ya kuelea nchini Marekani.
Mpango ulikuwa umekwishapita, walichokifanya siku hiyo ni kwenda kwenye kituo kikubwa cha upokeaji na usambazaji madawa, MSD (Medical Store Departiment) na kisha kuanza kujitambulisha kama madaktari wakubwa ambao walikuwa wametoka nchini Marekani kwa nia ya kuja hapa kwa ajili ya kuwafanyia tiba watoto.
Wasimamizi hawakuonekana kufahamu kitu chochote kile, mbaya zaidi wala hawakuomba hata vitambulisho kutokana na kiasi kikubwa cha fedha kutolewa kwa kila aliyekuwa na nia ya kuomba vitambulisho vyao hasa katika ngazi za chini.
Kila mtu ambaye alikuwa akipewa fedha, alikuwa akiwaruhusu kufanya mambo mengine ambayo wala hayakutakiwa kufanywa kwa mtu yeyote ambaye hakuonyesha kitambulisho cha kumjulisha kama alikuwa daktari.
“Madawa hayatoki mpaka nivione vitambulisho vyao” Mkuu wa usambazaji madawa katika kitengo hicho, mzee Samweli alimwambia msaidizi wake.
“Ila mkuu inab.....”
“Nimesema hakuna. Kama wao ni madaktari iliwabidi waje na madawa yao kama watu wengine wanavyofanya. Wanakuja huku halafu dawa wanategemea kwetu, hauoni kama huu ni ujinga?” Mzee Samweli aliuliza.
“Kama ukiangalia, unaweza kusema ni ujinga, ila naomba ujifikirie mkuu, ni mara ngapi tumekuwa na vitu hapa nchini halafu tukashindwa kuvitumia? Wape nafasi waokoe roho za watoto wetu” Mrisho alimwambia mzee Samweli.
“Sasa wao wameigia ndani ya nchi yao kama nani? Mbona hatujasikia taarifa za ujio wao?” Mzee Samweli aliuliza.
“Wamesema kwamba walipokuja hapa hawakuja kama madaktari bali walikuja kama watalii mkuu” Msaidizi, Mrisho alimwambia Samweli.
“Kumbe ni watalii! Sasa utalii na udaktari unaingiliana vipi hapo?” Mzee Samweli aliuliza.
“Wao ni madaktari ambao wamekuja huku kwa ajili ya kufanya utalii kama sehemu ya mapumziko yao ya likizo. Walipofika hapa, wamesikitishwa na hali waliyoikuta hasa kwa watoto. Kwa hiyo sasa, wameamua kuuvua utalii na kuuweka pembeni na kisha kuuvaa udaktari wao na kuingia kazini huku wakiwa na lengo moja tu, kuwanusuru watoto wetu ambao wapo katika matatizo makubwa hasa katika kipindi cha ukuaji” Mrisho alielezea kwa kirefu.
“Hebu waite kwanza niwaone” Mzee Samweli alimwambia Mrisho ambaye aliwaita Reuben na wenzake ndani ya chumba kile.
Mazungumzo yakaanza upya ndani ya chumba kile. Reuben na wenzake walikuwa wamevaa nyuso za bandia, nyuso ambazo zilikuwa zikionyesha kwamba walikuwa na uhitaji wa kuwasaidia watoto wa Kitanzania ambao walikuwa wakikua huku wakishambuliwa na magonjwa mbalimbali. 
Japokuwa walikuwa wakiongea mengi na kukubalika lakini wakaona kwamba kulikuwa na kitu cha ziada ambacho kilitakiwa kufanyika zaidi, umwagaji wa fedha ndani ya ofisi hiyo. Hawakutaka kuchelewa, walianza kujiumauma mwisho wa siku noti za dola mia moja zikawekwa mezani. Kwa haraka haraka mzee Samweli akazichukua na kuanza kuziangalia, zilikuwa noti za dola mia moja zilizokuwa kumi.
Kiasi cha dola elfu moja kilionekana kuwa kiasi kikubwa hasa kwa mtanzania kama mzee Samweli ambaye maisha yake yalikuwa yakitegemea sana mshahara wa kawaida. Wala hakutaka kujiuliza kama alitakiwa kuzichukua au kuziacha, alichokifanya ni kuziingiza mfukoni.
“Mrisho, hebu wapeleke stoo na kisha wape watakachokihitaji” Mzee Samweli alimwambia Mrisho ambaye alifanya kama alivyoambiwa.
Kwa Mtanzania, fedha ndio ilikuwa kila kitu, uwepo wa fedha ulikuwa na nafasi kubwa ya kubadilisha mambo mengi ambayo wala yasingeweza kubadilishwa. Fedha ikaonekana kuwa kila kitu, fedha hizo hizo ndizo ambazo zilikuwa zikiwafanya Reuben na wenzake kupelekwa katika stoo ya madawa ambako huko wakachagua madawa wanayoyataka na kisha kuondoka.
Kazi ilikuwa imebaki moja tu, kwanza ilibidi kwenda katika serikali ya mtaa wa Masaki na kuelezea kile ambacho kilikuwa kimewaleta mahali pale, walipofika huko, walimwaga kiasi kidogo cha fedha na wakaruhusiwa kufanya kazi zao katika mtaa huo.
Hawakuishia hapo, napo wakaenda mpaka katika hospitali ya Halmashauri iliyokuwepo Masaki na kisha kuongea na uongozi wa hospitali ambao ulionekana kuwa na furaha kupita kawaida, Reuben, Filbert na Endrew wakakaribishwa kuanza kufanya kazi katika hospitali hiyo.
Matangazo yakaanza kufanyika mitaani kwamba kulikuwa na chanjo ambayo ilikuwa ikitolewa kwa watoto waliokuwa chini ya miaka mitano na hivyo wazazi wao walitakiwa kuwapeleka watoto wao wao wenyewe kutokana na kutakiwa kuulizwa maswali mengi kuhusiana na watoto, chanjo hiyo ilitakiwa kufanyika siku inayofuatia.
“Nitampeleka Genuine huko huko kesho asubuhi” Prisca alimwambia mumewe, Gibson.
“Ni vizuri sana. Usimwache mfanyakazi ampeleke, si umesikia kwamba ni mzazi mwenyewe ndiye anayetakiwa kumpeleka?”
“Nimesikia mume wangu. Nitampeleka tu. Si wamesema mwisho jioni? Nitahakikisha nampeleka hata saa kumi” Prisca alimwambia Gibson.
“Hapana mpenzi. Nenda uko hata asubuhi. Usikawie, hauwezi kujua wingi wa watu. Wahi zako asubuhi tu” Gibson alimwambia Prisca.
“Sawa. Usijali mume wangu” Prisca aliitikia na kulala huku akiwa na hamu ya kumpeleka mtoto wake akapatiwe chanjo ya kumkinga na magonjwa mbalimbali katika kipindi chake cha ukuaji.

Je nini kitaendelea?
Je Katie atakamilisha mpango wake?

IMEDHAMINIWA NA FACEBOOK TAKE AWAY,ZANNEL BONGO LADIES WEAR,MAC AUTO ACCESSORIES,DICK SOUND.

No comments:

Post a Comment